Moi Avenue
Wakazi wa eneo la pembeni mjini Mombasa asubuhi ya leo walipigwa na mshtuko pale walipopata jamaa mmoja mwendesha teksi amekufa ndani ya gari lake. Polisi waliofika kukagua mwili huo hawakupata chochote ambacho kingaliashiria sababu ya kifo chake. Kisa hicho kilifanyika katika barabara kuu ya Moi Avenue eneo la pembeni.



